Madereva wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakimsikiliza Naibu Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua mafunzo elekezi kwa madereva hao yaliyofanyika Kibaha mkoani Pwani.
Waziri wa Katiba na Sheria akiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Wakili wa Serikali baada ya kufungua mafunzo kwa Mawakili hao yaliyogfanyika Jijini Arusha.
Mawakili wa Serikali wakimsikiliza Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Dkt. Juma Homera wakati akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika Jijini Arusha.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo akizungumza na viongozi wa Jumuiya ya Maridhiano na Amani Tanzania (JMAT) alipowasili kwenye viwanja vya Maonesho ya Kimataifa vya Mwalimu Nyerere kutembelea Maonesho ya 50 ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba) yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhusu Hassan akipokea maelezo kutoka kwa Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi kuhusu namna Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali inavyotekeleza majukumu yake wakati wa Ufunguzi wa Mkutano wa Chama cha Mawakili wa Serikali Tanzania (TPBA) uliofanyika Jijini Arusha.