Muonekano wa jengo la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali linaloendelea kujengwa katika Mji wa Serikali, Mtumba, Dodoma.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi (aliyesimama Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kabla ya kikao cha kutathmini utendaji kazi wa Ofisi hiyo kilichofanyika jijini Dodoma. Kushoto ni Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi akiangalia ramani ya jengo la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo unaoendelea katika Mji wa Serikali, Mtumba, Dodoma.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo akifuatilia majadiliano ya kikao cha menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali cha kutathmini utendaji kazi wa Ofisi hiyo kilichofanyika jijini Dodoma.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi akiendesha kikao cha menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali cha kutathmini utendaji kazi wa Ofisi hiyo kilichofanyika jijini Dodoma.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi (wa pili kushoto) akipatiwa maelezo na mkandarasi, Meneja Ujenzi Kanda ya Mashariki wa SUMA JKT, Kanali Saul Chiwanga kuhusu maendeleo ya ujenzi wa jengo la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa ziara yake ya kukagua jengo hilo lililopo Mji wa Serikali, Mtumba, Dodoma.