Waajiriwa wapya wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakimsikiliza kwa makini Dkt. Boniphace Luhende, Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifunga mafunzo elekezi kwa wajiriwa hao kuhusu sheria, taratibu na kanuni za utumishi wa umma yaliyofanyika Mkoani Pwani.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti ya OWMS wakimsikiliza kwa makini Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende wakati akifunga mafunzo elekezi kwa waajiriwa wapya wa Ofisi hiyo yaliyofanyika Kibaha mkoani Pwani.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Menejimenti na waajiriwa wapya wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali baada ya kufunga mafunzo elekezi kwa watumishi hao yaliyofanyika Kibaha.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Sarah Mwaipopo (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na waajiriwa wapya wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali baada ya kufungua mafuzo elekezi kwa watumishi hao yaliyofanyika Kibaha mkoani Pwani.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende (wa tatu kulia) akimuonesha vitabu vya mashauri ya usuluhishi Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Pauline Gekul (wa pili kulia) alipotembelea Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Sarah Mwaipopo (aliyesimama katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanawake wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kumaliza kikao kifupi kwa ajili ya kujadili kauli mbiu ya Siku ya Wanawake Duniani.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende akiwa kwenye picha ya pamoja na Kaimu Mtendaji Mkuu wa TLS, Bi. Mariam Othman na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Sarah Mwaipopo pamoja na viongozi wengine wa Ofisi hizo mara baada ya kikao baina yao.
Baadhi ya wajumbe wa Menejimenti na Maafisa Bajeti wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakiandaa bajeti ya Mwaka wa Fedha 2023/24 kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere kilichopo Kibaha mkoani Pwani
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Mhe. Sarah Duncan Mwaipopo (aliyesimama katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mawakili wa Serikali wa Ofisi yake kwenye maadhimisho ya Kilele ya Wiki ya Sheria
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Mhe. Sarah Duncan Mwaipopo akiwa kwenye picha ya pamoja na Katibu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mary Makondo wakati wa Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Sheria yaliyofanyika leo Jijini Dodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Dkt. Eliezer Mbuki Feleshi akisoma hotuba yake katika Sherehe za Maadhimisho ya kilele cha Siku ya Sheria nchini yaliyofanyika Jijini Dodoma.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akizungumza na viongozi na watumishi pamoja na wananchi (hawapo pichani) walioshiriki sherehe za kilele cha Siku ya Sheria nchini leo tarehe 01 Februari, 2023 jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali pamoja na Majaji walioshiriki Maadhimisho ya Kilele cha Wiki ya Sheria Tanzania yaliyofanyika tarehe 1 Februari, 2023 Jijini Dodoma
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende akizungumza na Rais wa Taasisi ya Usuluhishi Tanzania Bi. Madeline Kimei (hayupo pichani) alipotembelea Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujitambulisha.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende (kushoto) akimkabidhi Jarida la Wakili Mkuu Rais wa Taasisi ya Usuluhishi Tanzania, Bi Madeline Kimei alipofika Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali jijini Dar es Salaam kwa lengo la kujitambulisha.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi Sarah Mwaipopo (aliyesimama kushoto) na Rais wa Taaisisi ya Usuluhishi Tanzania, Bi. Madeline Kimei baada ya kumaliza kikao.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Sarah Mwaipopo akizungumza na Mawakili Wafawidhi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali waliopo mkoani Tanga wakati wa kikao kilichofanyika kwa njia ya mtandao cha kujadili utekelezaji wa majukumu ya Ofisi hiyo.
Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akisalimiana na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende mara baada ya kuwasili kwenye ukumbi wa mikutano wa Jakaya Mrisho Kikwete, Jijini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan,akimuapisha Sarah Duncan Mwaipopo kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Dkt. Boniphace Nalija Luhende kuwa Wakili Mkuu wa Serikali, katika hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Dkt. Boniphace Luhende Wakili Mkuu wa Serikali akiwa kwenye picha ya pamoja na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Sara Mwaipopo, na wajumbe wa Menejimenti wa Ofisi hiyo baada ya viongozi hao kuwasili Ofisini hapo muda mfupi baada ya kuapishwa.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende akizungumza na wajumbe wa Baraza la Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akifungua Mkutano wa Kwanza wa Baraza la Wafanyakazi la Ofisi hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 kwa mwaka wa fedha 2022/23.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Slyvester Mwakitalu, akizungumza na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo vya Sheria kutoka Wizara, Taasisi za Umma, Mashirika ya Umma na Halmashauri zote nchini wakati wa kikao kazi chao kilichofanyika Jijini Dodoma.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Jaji. Dkt. Eliezer Feleshi akifungua kikao kazi cha Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo vya Sheria wa Wizara mbalimbali, Taasisi za Umma, Mashirika ya Umma na Halmashauri zote nchini kilichofanyika Jijini Dodoma.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akizungumza na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo vya Sheria kutoka Wizara , Taasisi, Mashirika ya Umma na Halmashauri zote nchini wakati wa kikao kazi kilichofanyika Jijini Dodoma.
06th May 2023
Watumishi wapya wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OWMS) wametakiwa kutumia elimu waliyoipata na fursa ya ajira ya Serikali kutekeleza majukumu yao... Soma zaidi
Soma zaidi