Kaimu Mkurugenzi wa Mashauri na Udhibiti Ubora, ndugu Camilius Ruhinda (aliyesimama katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati wa maonesho ya SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo akitazama moja ya bidhaa inayopatikana ndani ya banda la Zanzibar alipotembelea banda hilo kwenye Maonesho ya SabaSaba ya jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo akipokea zawadi ya jarida na vipeperushi kutoka kwa Afisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA, Bi. Asiatu Msuya baada ya kutembelea banda la Ofisi hiyo kwenye Maonesho ya SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo akimsikiliza Afisa Uhusiano Mwandamizi wa EWURA, Bi. Asiatu Msuya alipotembelea banda la Ofisi hiyo kwenye Maonesho ya SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo (aliyesimama katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali alipotembelea banda la Ofisi hiyo kwenye Maonesho ya SabaSaba jijini Dar es Salaam.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende akitoa maoni kuhusu Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 alipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 wakati wa mahojiano yaliyofanyika Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Boniphace Luhende (aliyesimama katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050 baada ya kutoa maoni ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (aliyeketi katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Watumishi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa Serikali yanayofanyika Jijini Arusha.
Mawakili wa Serikali wanaoshiriki Mafunzo ya siku tatu wakimsikiliza Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo hayo yanayofanyika jijini Arusha.
Mkurugenzi Msaidizi Menejimenti ya Usimamizi wa Mashauri Ndg. Camilius Ruhinda akitoa mada kuhusu namna ya kukabiliana na viashiria hatarishi katika uendeshaji wa mashauri ya Madai na Usuluhishi wakati wa mafunzo ya siku tatu yanayofanyika jijini Arusha.
Mwezeshaji wa Mafunzo Bi. Stella Mrosso akitoa mada kuhusu Uhakiki Ubora katika kuendesha Mashauri ya Madai na Usuluhishi kwa mawakili wa Serikali wakati wa mafunzo ya Siku Tatu yanayofanyika Jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) akizindua nembo ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa Mawakili wa Serikali jijini Arusha.
Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Bi. Alice Mtulo akizungumza na Mawakili wa Serikali wakati wa mafunzo kwa Mawakili hao yanayofanyika Jijini Arusha.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akitoa salamu za Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakati akimkaribisha Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) aweze kufungua mafunzo ya mawakili wa serikali yanayofanyika jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (aliyeketi katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mawakili wa Serikali kutoka Afisi ya Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Mawakili wa Serikali Jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) akizungumza na Mawakili wa Serikali wakati akifungua mafunzo ya siku tatu kwa mawakili wa serikali yanayofanyika jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini (Mb) akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua mafunzo ya siku tatu kwa Mawakili wa Serikali Jijini Arusha.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua mafunzo kuhusu Haki na Wajibu wa Watumishi katika Utumishi wa Umma mkoani Morogoro.
Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali wakimsikiliza Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Boniphace Luhende (Hayupo pichani) wakati akifungua mafunzo kuhusu Haki na Wajibu wa Watumishi katika Utumishi wa Umma mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akiwa kwenye picha ya pamoja na wajumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali uliofanyika mkoani Morogoro.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Jumanne Sagini akiwa kwenye picha ya pamoja na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya kufungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi hiyo Mkoani Morogoro.
Wakili Mkuu wa Serikali Dkt. Bonipace Luhende akiwa kwenye picha ya pamoja na Mawakili Wafawidhi wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali mara baada ya ya kufungua Mafunzo kuhusu Usimamizi wa Mashauri na Udhibiti Ubora yanayoendelea Kibaha mkoani Pwani.
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Dkt. Eliezer Feleshi akizungumza na washiriki wa Mafuzo Elekezi kuhusu Uendeshaji wa Mashauri na Udhibi Ubora wakati akifungua mafunzo hayo yanayoendelea Kibaha mkoani Pwani.
Baadhi ya Makatibu Sheria wa OWMS wanaoshiriki Mafunzo Elekezi kuhusu Matumizi ya Mfumo Mpya wa Mahakama wa Kusajili na Kuratibu Mashauri (e-CMS) wakifuatilia mada kuhusu namna mfumo huo unavyofanya kazi.
Kaimu Naibu Wakili Mkuu wa Serikali Ndg. Mark Mulwambo (kulia) akizungumza na Makatibu Sheria wa OfWMS wakati akifungua Mafunzo Elekezi kuhusu Matumizi ya Mfumo Mpya wa Mahakama wa Kusajili na Kuratibu Mashauri (e-CMS) yaliyofanyika Mkoani Morogoro.
22nd May 2024
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Jumanne Sagini amewataka Mawakili wa Serikali kutoa ushauri mapema kabla mambo hayajaharibika. Soma zaidi
Soma zaidi