Wakili Mkuu wa Serikali, Dkt. Ally Possi amefungua kikao kazi cha wadau wa Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali (OWMS) cha kupitia na kutoa maoni kuhusu Kanuni za Urejeshaji wa Gharama za Uendeshaji Mashauri ya Serikali kilichofanyika mkoa wa Pwani.
Soma zaidiWananchi wametakiwa kuendelea kupata elimu kuhusu uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu licha la Mahakama kuruhusu waleta maombi katika shauri linalopinga mamlaka ya Waziri wa TAMISEMI kutunga kanuni za kuratibu, kusimamia nakuendesha uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini kuruhusiwa kufungua shauri la msingi kwa kuwa mchakato mzima wa uchaguzi haujasimamishwa.
Soma zaidiWajumbe wa Menejimenti ya Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali kutekeleza majukumu yao kwa kushirikiana hatua itakayowasaidia kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kufikia malengo yao waliyojiwekea ndani ya muda ulipangwa.
Soma zaidiOfisi ya Wakili Mkuu wa Serikali ikiwa ndio yenye dhamana ya kusimamia, kuratibu na kuendesha mashauri ya Madai na Usuluhishi ndani na nje ya nchi imeokoa jumla ya Sh bilioni 602.52, dola za kimarekani milioni 800.2 na euro milioni mbili ambazo serikali ingetakiwa kulipa kama serikali ingeshindwa katika mashauri mbalimbali yaliyofunguliwa ndani na nje ya nchi.
Soma zaidiOfisi ya Wakili Mkuu wa Serikali itaendelea kushirikiana na Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) kwa lengo la kuendelea kuisaidia Serikali kutekeleza majukumu yake kwa kuangalia namna gani itatumia taaluma ya sheria kwa maslahi ya Taifa ili kuvutia wawekezaji wa sekta mbalimba nchini.
Soma zaidi